Psalms 18:37-42


37 aNiliwafuatia adui zangu na nikawapata,
sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.

38 bNiliwaseta hata hawakuweza kuinuka tena;
walianguka chini ya miguu yangu.

39 cUlinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita;
uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.

40 dUliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia,
nami nikawaangamiza adui zangu.

41 eWalipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa;
walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.

42 fNiliwaponda kama mavumbi yanayopeperushwa na upepo;
niliwamwaga nje kama tope barabarani.

Copyright information for SwhKC